Haturuhusu Wenyeji wawe na kamera za usalama au vifaa vya kurekodi vinavyofuatilia sehemu za ndani, hata ikiwa vifaa hivi vimezimwa. Kamera zilizofichwa zimepigwa marufuku kila wakati na zitaendelea kupigwa marufuku. Wenyeji wanaruhusiwa kuwa na kamera za usalama za nje, vifuatiliaji vya kiwango cha sauti na vifaa mahiri ili mradi wazingatie miongozo ifuatayo na sheria zinazotumika.
Sheria hizi zinaanza kutumika tarehe 30 Aprili, 2024.